Beda Achaguliwa Mwenyekiti CCM Katavi
Katavi
Aliyekuwa mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mpanda amechaguliwa kuwa mwenyekiti mpya wa chama hicho mkoa wa Katavi
Bwana Beda Katani amechaguliwa jana katika mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa Skylux Marando akimshinda mpinzani wake Eneck Gwambasa aliyewahi kuwa mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Mpanda
Wengine waliochaguliwa ni pamoja na Girbet Jordani kuwa mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa.
Msimamizi wa uchaguzi huo alikuwa mkuu wa wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma Deo Denjembi
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni