![]() |
| tuzo aliotunukiwa Millen |
Mwanamitindo na Mrembo wa
Tanzania mwaka 2001, Happiness Millen Magese ametunukiwa tuzo ya pekee ya BET
mwaka huu iitwayo ‘Global Good Award’
Millen amepewa tuzo hii kutokana na jitihada zake za kampeni ya
ugonjwa wa endometriosis (ugonjwa unaosababishwa na seli za tumbo la uzazi kuwa
nje ya kizazi) ambao amekuwa nao katika maisha yake yote tangu awe msichana.
Millen ameanzisha taasisi
ya kuwasaidia wanawake wengine hapa
nchini ya Millen Magese Faundation ili waepuke kile ambacho kilimkuta yeye. Pamoja
na hivyo Millen amekuwa mstari wa mbele kutoa misaada mbalimbali kwa
wasiojiweza.
![]() |
| Eddy Kenzo kwenye red carpet akiwa na wapambe |
Katika tuzo hizo pia msaani
wa Uganda Eddy Kenzo amebeba tuzo ya msanii bora mpya wa kimataifa anayependwa
na watazamaji (Viewer’s Choice Best New International Artist, 2015)
Kaitka kipengele hicho Eddy
Kenzo alikuwa akichuana na Assper Nyovest wa Afrika kusini, Mz Vee wa Ghana na
wasanii wa uingereza, George the poet, MIC Lowry Na Novelist
Kenzo katika ukurasa wake
wa facebook amewashukru washabiki wake, huku akisema ilikuwa ni safari ndefu na
akasema ni tuzo ya pekee kwa ukanda wa Afrika Mashariki.





