Ijumaa, 20 Aprili 2018

Taasisi Marekani Kuendeleza Kikapu nchini


Taasisi ya maendeleo ya Mpira wa Kikapu🏀 inayomilikiwa na Kocha wa klabu ya San Fransisco  kwa kushirikiana Jamtown Gym na wadau wengine wa Marekani wamekubali kushirikiana na Chama cha mpira wa Kikapu nchini (TBF) kuendeleza mchezo huo nchini.

Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya Rais wa TBF Phares Magesa kufanya ziara ya Kikazi nchini humo na kukutana na Kocha wa San Fransisco, Ameer Aziz ambaye wamekbaliana kuendesha mafunzo kwa vijana wadogo.

"miongoni mwa tuliyokubaliana ni kuendesha mafunzo kwa vijana wadogo , mafunzo hayo yatafanyika Tanzania na pia Marekani ambapo baadhi ya vijana watapatiwa nafasi za kufanya mafunzo Marekani na pia vijana wa Marekani watatembelea Tanzania kufanya mafunzo na vijana wetu,  timu yetu ya Taifa ya Vijana itapatiwa nafasi ya kujifunza zaidi Marekani na kupewa michezo ya majaribio na timu nyingine za mataifa mengine ambazo nazo zitaalikwa kutoka mabara mengine katika mashidano maalumu, kutoka Afrika ni Tanzania pekee ndio tumepewa nafasi hiyo" Alisema Magesa.

Ameongeza kuwa Taasisi hiyo itakuwa inasaidia kuratibu upatikanaji wa vifaa vya michezo Marekani na kuvileta Tanzania, pamoja na kutafuta wafadhili watakaoweza kusaidia utekelezaji wa programs za maendeleo ya kikapu ili kukuza mchezo huu nchini.

Mbalo na hayo ushirikiano huo pia utashuhudia wachezaji kadhaa nyota wa kikapu duniani wakitua nchini kuendesha Clinics za kikapu.
Ameongeza kuwa Tanzania itafaidika na kuratibu mradi wa ujenzi wa viwanja vya kikapu nchini, kutoa nafasi ya mafunzo kwa Timu zetu zote za Taifa kufanya mafunzo maalumu katika Gym ya Jamtown iliyoko Oakland, California.

"Timu zetu zitapata nafasi kutumia Gym bora kuliko zote hapa Marekani na inatumiwa pia na wachezaji wengi mahiri kwa mazoezi binafsi wakiwemo Stephen Curry na Kelvin Durant,Taasisi hii pia itaratibu na kujenga ushirikiano kati ya timu za Tanzania na baadhi ya timu mahiri za NBA ikiwemo timu ya Golden State Warriors".Aliongeza Magesa.
Aidha amewataka wadau nchini kushirikiana na TBF katika maendeleo ya Mchezo wa Kikapu.

TBF ipo kwenye maandalizi ya kuandaa michuano ya Kanda ya Tano kwa vijana wenye umri chini ya miaka 18 (FIBA Zone V U18) itakayofanyika June 2018 jijini Dar es Salaam.
🏀

Jumatano, 6 Desemba 2017

Beda Achaguliwa Mwenyekiti CCM Katavi

Katavi

Aliyekuwa mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mpanda amechaguliwa kuwa mwenyekiti mpya wa chama hicho mkoa wa Katavi

Bwana Beda Katani amechaguliwa jana katika mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa Skylux Marando akimshinda  mpinzani wake Eneck Gwambasa aliyewahi kuwa mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Mpanda

Wengine waliochaguliwa ni pamoja na Girbet Jordani kuwa mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa.

Msimamizi wa uchaguzi huo alikuwa mkuu wa wilaya ya Kongwa  mkoani Dodoma Deo Denjembi

Rais Magufuli Ateua Wenyeviti Wa Bodi 6

Na, IKULU
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wenyeviti wa bodi 6 za taasisi za Serikali baada ya wenyeviti waliokuwepo kumaliza muda wao.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 06 Desemba, 2017 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Kwanza Mhe. Rais Magufuli amemteua Bi. Monica Ngenzi Mbega kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mazao Mchanganyiko kuanzia tarehe 30 Novemba, 2017.
Pili, Mhe. Rais Magufuli amemteua Prof. Egid Beatus Mubofu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) kuanzia tarehe 01 Desemba, 2017.
Tatu, Mhe. Rais Magufuli amemteua Prof. Abiud Kaswamila kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro kuanzia tarehe 01 Desemba, 2017.
Nne, Mhe. Rais Magufuli amemteua Prof. Esther Hellen Jason kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kuanzia tarehe 01 Desemba, 2017.
Tano, Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Kenneth Mdadila kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya taasisi ya kifedha ya Self Microfinance Fund Limited kuanzia tarehe 01 Desemba, 2017.
Sita, Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Titus Mlengeya Dismas Kamani kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania kuanzia tarehe 06 Desemba, 2017.

Jumanne, 29 Desemba 2015

MAJI NI UHAI!!, MAJI NI KIFO.

Katika maisha ni vigumu kukua bila kusikia ili neno, “maji ni uhai”  katika hali halisi ya dhana maji ni uhai tunaambiwa maji uchukua asilimia kubwa ya mwili wa binadamu pia maji kwa kiasi kikubwa ndio yamezunguka uso wa dunia.

mkufunzi wa uogeleaji akiwa na wanafunzi katika mazoezi
Maji ni uhai kwa kuwa mwili wa binadamu una uhuitaji wa maji pia viumbe hai vyote kwa kiasi kikubwa utegemea maji ili viishi. Lakini maji pia ni chanzo cha kupotea kwa uhai kwa viumbe hawa ambao utegemea sana maji.

Dunia imeshuhudia vifo vingi vya maji inapotekea majanga kama kuzama kwa meli, mashua na boti, lakini pia inapotokea mafuriko. Majanga haya ugharimu maisha ya watu wengi zaidi. Lakini pia uzembe wa kutofunika baadhi ya mashimo hama vyombo vya maji navyo vimekuwa vikigharimu uhai.

Kumekuwa na matukio mengi ya watu kudumbukia kwenye madibwi na kupoteza maisha ila pia watoto majumbani kufariki kwa kudumbukia kwenye vyombo vyenye maji ama visima.
Kama maji ni uhai je kwa nini vifo hivi vinatokea? Jibu la swali hili linaweza kuwa gumu kidogo lakini kwa jibu la kawaida ni kuwa kila chenye uzuri hakikosi ubaya au wengine wanasema ukizidisha kilakitu kinakuwa sumu.

Maana yake ni kuwa maji yasipotumiwa vizuri yaani kuchukua tahadhari na kujua hatari za maji bhasi ni chanzo kikubwa cha kupotea kwa maisha.
boya la kuokolea
Je vifo vya maji ni mpango wa Mungu?
Stewart Kiluswa mkufunzi wa uogeleaji kwa kujiokoa na kuokoa maisha, anasema, vifo vingi vya maji hutokea kutokana na uzembe na kutokujua hatari za maeneo watu wanamoishi au jinsi ya kujioka na hatari za maji.

Unawezaje  kutambua hatari za maji na jinsi gani ya kujikinga nazo.
Kujua hatari za maji ni vyema kuwa na mwenyeji au kuuliza wenyeji  hali halisi ya mazingira ya maji uliopo, kama kuna wanyama wakali, mikond mkali wa bahari au kama kuna alama kataza (zinazozuia) matumizi ya eneo hilo. Pia kuwa waangalifu na vyombo vya maji kama ndoo na baseni hasa hasa tunapokuwa na watoto wadogo, pia kuhakikisha mazingira yetu yenye mashimo makubwa yanawekea alama za tahadhari ili kuzuia majanga. Mara nyingi watoto upenda kwenda kucheza wakiwa peke yao ni vyema kujua wanachezea maeneo gani na kama ni eneo la maji ni vyema wakawa na uangalizi wa mkubwa.
mmoja wa wanaojifinza kuogelea

Jinsi  ya kujiokoa na kuokoa mtu aliye katika hatari ya kufa maji.
Kuna aina ya watu wane wanaokuwa katika hatari ya kufa maji nao ni:
Asiyejua kuogelea kabisa, anayejua kuogelea kidogo, anayejua kuogelea  na aliyepoteza fahamu majini

Asiyejua kuogelea  huyu mara nyingi akiwa katika hatari ya kufa maji huzama na kuibuka akiwa katika hali ya wima, ilihali anayejua kuogelea kidogo huzama na kuibuka akiwa katika hali ya mshazali na mara nyingi hujitahidi kuelekea sehemu ambayo anaweza kupata musaada kwa haraka, huyu ujitahidi kujaribu kuogelea ndio maana huwa  katika hali ya mshazali.

Anayejua kuogelea, anaweza kuwa katika hatari ya kufa maji kutokana na sababu kama kushambuliwa na wanyama au wadudu wa majini na hvyo akili yake yote uhiamishia palipo na jeraha ila pia anaweza kuwa amebanwa na matatizo ya msuli hivyo vyote vinaweza kupelekea maisha ya mtu kuwa hatarini kwenye maji.

Aliyepoteza fahamu huyu ni kwamba anakuwa ajitambui na mwili wake unaweza kuwa unaelea au umezama chini.

Wakati wa kuwapatia msaada wa uokozi jitahidi sana kutokumgusa mtu ambaye bado ni mzima yaani ajapoteza fahamu. Tumia nyenzo yoyote ile ambayo ataweza kuishika na ww kumvuta kwa kutumia hyo nyenzo, mfano wa nyezo za  uokozi ni kama maboya, mti mrefu, kamba au kidumu chenye mfuniko kilichofugwa kamba au nguo au kitu chochote kinachoelea, kumbuka wakati unajaribu kuokoa hakikisha maisha yako ni salama. Kwa mtu ambaye amepoteza fahamu unaweza kumfikia na kumshika wakati wa kumtoa kuelekea nchi kavu.


Maji ni uhai ila pia maji ni chanzo cha vifo, tujihadhari katika matumizi ya maji.

Jumamosi, 11 Julai 2015

MMOJA ASHIKILIWA NA POLISI KUELEKEA MKUTANO MKUU CCM

Polisi Dodoma inamshikilia mtu mmoja mwenye asilia ya Asia akiwa na kiasi kikubwa cha fedha, ahusishwa na mchakato wa mchujo unaondelea.
Raia anaedaiwa kukamatwa, pamoja na fedha alizokutwa nazo

katika mitandao ya kijamii picha za mtu huyo zimesambaa sana huku akihusishwa na mmoja wa wagombea walio katika tano bora, Bernard Membe.

Akielezea sintofahamu hiyo, Bernard Membe ameandika katika ukurasa wake wa twitter akisema, "Kuna taarifa za uongo zinazoenezwa kwamba kuna "Mtu wa Membe" amekamatwa na pesa Dodoma,siasa hizi ni za hovyo kwani hazitajenga Taifa letu. Naomba msihadaike na watu wanaotaka kututia doa baada ya kukosa uchafu dhidi yetu"

LOWASA AKATWA TANO BORA CCM

hatimaye kitendawili cha nani yumo nani kakatwa kimeteguliwa, huku waziri mkuu wa zamani ambaye alijizolea wadhamini wengi, Edward Lowasa akiwa amewekwa pembeni.

Tano bora iliyopitishwa na kamati kuu ya CCM ni Bernard Membe, Dr. John Magufuli, Asha Rose Migiro, January Makamba na Amina Salum Alli.

Baada ya vikao vya kamati kuu ya Chama cha Mapinduzi (CC) kukaa kwa muda mrefu bila ufumbuzi wa tano bora, huku nchi nzima ikielekeza macho yao mjini Dodoma ambapo vikao hivyo ndo vinafanyika.

katibu uenezi wa chama hicho Nape Nauye amesema majina hayo yatapelekwa halimashauri kuu taifa ambayo ndio itatoa tatu bora kabla ya mkutano mkuu hapo baadae leo hii.



Jumanne, 7 Julai 2015

MBUNGE CHADEMA ANUSURIKA, AJALI YA HELIKOPITA

helikopita baada ya kuanguka.
Mbunge wa Arumeru Mashariki,mkoani Arusha Joshua Nassari amepata ajali ya helkopta aliyokua anaitumia kufanya ziara katika jimbo lake.

Habari za awali tulizozipata ni kwamba mbunge huyo wa Chadema Joshua Nassari amenusurika kufa baada ya Helkopta aliyokuwa anaitumia kuanguka baada ya kunasa kwenye mti baada ya kupotea kwenye mawingu.


Aidha taarifa hizo zinaeleza kuwa Mbunge huyo kwa Tiketi ya Chadema, na rubani wake walitoka wakiwa wazima na wapo katika Hospitali ya Kanisa la Kilutheri ya Selian ya jijini Arusha. 
Mbunge wa Arumeru mashariki, Joshua Nassari akiwa na helicopita aliyopata nayo ajali