Jumanne, 29 Desemba 2015

MAJI NI UHAI!!, MAJI NI KIFO.

Katika maisha ni vigumu kukua bila kusikia ili neno, “maji ni uhai”  katika hali halisi ya dhana maji ni uhai tunaambiwa maji uchukua asilimia kubwa ya mwili wa binadamu pia maji kwa kiasi kikubwa ndio yamezunguka uso wa dunia.

mkufunzi wa uogeleaji akiwa na wanafunzi katika mazoezi
Maji ni uhai kwa kuwa mwili wa binadamu una uhuitaji wa maji pia viumbe hai vyote kwa kiasi kikubwa utegemea maji ili viishi. Lakini maji pia ni chanzo cha kupotea kwa uhai kwa viumbe hawa ambao utegemea sana maji.

Dunia imeshuhudia vifo vingi vya maji inapotekea majanga kama kuzama kwa meli, mashua na boti, lakini pia inapotokea mafuriko. Majanga haya ugharimu maisha ya watu wengi zaidi. Lakini pia uzembe wa kutofunika baadhi ya mashimo hama vyombo vya maji navyo vimekuwa vikigharimu uhai.

Kumekuwa na matukio mengi ya watu kudumbukia kwenye madibwi na kupoteza maisha ila pia watoto majumbani kufariki kwa kudumbukia kwenye vyombo vyenye maji ama visima.
Kama maji ni uhai je kwa nini vifo hivi vinatokea? Jibu la swali hili linaweza kuwa gumu kidogo lakini kwa jibu la kawaida ni kuwa kila chenye uzuri hakikosi ubaya au wengine wanasema ukizidisha kilakitu kinakuwa sumu.

Maana yake ni kuwa maji yasipotumiwa vizuri yaani kuchukua tahadhari na kujua hatari za maji bhasi ni chanzo kikubwa cha kupotea kwa maisha.
boya la kuokolea
Je vifo vya maji ni mpango wa Mungu?
Stewart Kiluswa mkufunzi wa uogeleaji kwa kujiokoa na kuokoa maisha, anasema, vifo vingi vya maji hutokea kutokana na uzembe na kutokujua hatari za maeneo watu wanamoishi au jinsi ya kujioka na hatari za maji.

Unawezaje  kutambua hatari za maji na jinsi gani ya kujikinga nazo.
Kujua hatari za maji ni vyema kuwa na mwenyeji au kuuliza wenyeji  hali halisi ya mazingira ya maji uliopo, kama kuna wanyama wakali, mikond mkali wa bahari au kama kuna alama kataza (zinazozuia) matumizi ya eneo hilo. Pia kuwa waangalifu na vyombo vya maji kama ndoo na baseni hasa hasa tunapokuwa na watoto wadogo, pia kuhakikisha mazingira yetu yenye mashimo makubwa yanawekea alama za tahadhari ili kuzuia majanga. Mara nyingi watoto upenda kwenda kucheza wakiwa peke yao ni vyema kujua wanachezea maeneo gani na kama ni eneo la maji ni vyema wakawa na uangalizi wa mkubwa.
mmoja wa wanaojifinza kuogelea

Jinsi  ya kujiokoa na kuokoa mtu aliye katika hatari ya kufa maji.
Kuna aina ya watu wane wanaokuwa katika hatari ya kufa maji nao ni:
Asiyejua kuogelea kabisa, anayejua kuogelea kidogo, anayejua kuogelea  na aliyepoteza fahamu majini

Asiyejua kuogelea  huyu mara nyingi akiwa katika hatari ya kufa maji huzama na kuibuka akiwa katika hali ya wima, ilihali anayejua kuogelea kidogo huzama na kuibuka akiwa katika hali ya mshazali na mara nyingi hujitahidi kuelekea sehemu ambayo anaweza kupata musaada kwa haraka, huyu ujitahidi kujaribu kuogelea ndio maana huwa  katika hali ya mshazali.

Anayejua kuogelea, anaweza kuwa katika hatari ya kufa maji kutokana na sababu kama kushambuliwa na wanyama au wadudu wa majini na hvyo akili yake yote uhiamishia palipo na jeraha ila pia anaweza kuwa amebanwa na matatizo ya msuli hivyo vyote vinaweza kupelekea maisha ya mtu kuwa hatarini kwenye maji.

Aliyepoteza fahamu huyu ni kwamba anakuwa ajitambui na mwili wake unaweza kuwa unaelea au umezama chini.

Wakati wa kuwapatia msaada wa uokozi jitahidi sana kutokumgusa mtu ambaye bado ni mzima yaani ajapoteza fahamu. Tumia nyenzo yoyote ile ambayo ataweza kuishika na ww kumvuta kwa kutumia hyo nyenzo, mfano wa nyezo za  uokozi ni kama maboya, mti mrefu, kamba au kidumu chenye mfuniko kilichofugwa kamba au nguo au kitu chochote kinachoelea, kumbuka wakati unajaribu kuokoa hakikisha maisha yako ni salama. Kwa mtu ambaye amepoteza fahamu unaweza kumfikia na kumshika wakati wa kumtoa kuelekea nchi kavu.


Maji ni uhai ila pia maji ni chanzo cha vifo, tujihadhari katika matumizi ya maji.

Jumamosi, 11 Julai 2015

MMOJA ASHIKILIWA NA POLISI KUELEKEA MKUTANO MKUU CCM

Polisi Dodoma inamshikilia mtu mmoja mwenye asilia ya Asia akiwa na kiasi kikubwa cha fedha, ahusishwa na mchakato wa mchujo unaondelea.
Raia anaedaiwa kukamatwa, pamoja na fedha alizokutwa nazo

katika mitandao ya kijamii picha za mtu huyo zimesambaa sana huku akihusishwa na mmoja wa wagombea walio katika tano bora, Bernard Membe.

Akielezea sintofahamu hiyo, Bernard Membe ameandika katika ukurasa wake wa twitter akisema, "Kuna taarifa za uongo zinazoenezwa kwamba kuna "Mtu wa Membe" amekamatwa na pesa Dodoma,siasa hizi ni za hovyo kwani hazitajenga Taifa letu. Naomba msihadaike na watu wanaotaka kututia doa baada ya kukosa uchafu dhidi yetu"

LOWASA AKATWA TANO BORA CCM

hatimaye kitendawili cha nani yumo nani kakatwa kimeteguliwa, huku waziri mkuu wa zamani ambaye alijizolea wadhamini wengi, Edward Lowasa akiwa amewekwa pembeni.

Tano bora iliyopitishwa na kamati kuu ya CCM ni Bernard Membe, Dr. John Magufuli, Asha Rose Migiro, January Makamba na Amina Salum Alli.

Baada ya vikao vya kamati kuu ya Chama cha Mapinduzi (CC) kukaa kwa muda mrefu bila ufumbuzi wa tano bora, huku nchi nzima ikielekeza macho yao mjini Dodoma ambapo vikao hivyo ndo vinafanyika.

katibu uenezi wa chama hicho Nape Nauye amesema majina hayo yatapelekwa halimashauri kuu taifa ambayo ndio itatoa tatu bora kabla ya mkutano mkuu hapo baadae leo hii.



Jumanne, 7 Julai 2015

MBUNGE CHADEMA ANUSURIKA, AJALI YA HELIKOPITA

helikopita baada ya kuanguka.
Mbunge wa Arumeru Mashariki,mkoani Arusha Joshua Nassari amepata ajali ya helkopta aliyokua anaitumia kufanya ziara katika jimbo lake.

Habari za awali tulizozipata ni kwamba mbunge huyo wa Chadema Joshua Nassari amenusurika kufa baada ya Helkopta aliyokuwa anaitumia kuanguka baada ya kunasa kwenye mti baada ya kupotea kwenye mawingu.


Aidha taarifa hizo zinaeleza kuwa Mbunge huyo kwa Tiketi ya Chadema, na rubani wake walitoka wakiwa wazima na wapo katika Hospitali ya Kanisa la Kilutheri ya Selian ya jijini Arusha. 
Mbunge wa Arumeru mashariki, Joshua Nassari akiwa na helicopita aliyopata nayo ajali

Jumamosi, 4 Julai 2015

BUNGENI HAKUKALIKI WANGINE WAPINGWA STOP

Kwa siku tatu mfululizo bunge limekuwa na mzozo ambao umekuwa ukipelekea kuahirishwa kwa vikao vya bunge huku, baadhi ya wabunge wakisimamishwa kuhudhuria vikao vilivyobaki vya bunge hilo ambalo linakoma July 8.

Alhamisi July 02 2015 Mbunge John Mnyika aliomba mwongozo kuomba Bunge lisiendelee kwa vile ishu ya kujadili Miswada mitatu iliyowasilishwa kwa hati ya dharura kwa siku moja ilikuwa inakiuka Kanuni za Bunge, ukatokea mvutano na baadae Spika Anne Makinda akaahirisha Bunge.

Ijumaa July 03 2015 hali ikawa hivyo hivyo tena, wakati Waziri George Simbachawene anasoma Muswada, ikatokea mvutano mwingine, zikaanzishwa kelele Bunge likaahirisha tena.. Kikao cha Jioni Spika Anne Makinda akarudi na list ya majina ya Wabunge ambao wamesimamishwa Bungeni kutokanana maamuzi ya Kamati ya Maadili ya Bunge. 

Leo July 04 2015 Kikao kimeanza tena saa tatu asubuhi, Mbunge Ezekiel Wenjeakaomba Spika atoe ufafanuzi wa kwanini Mbunge Silinde hayuko kwenye list ya waliotajwa kusimamishwa lakini Askari wa Bunge wamemzuia asiingie kwenye Kikao?

Majibu ya Spika hayakuwaridhisha baadhi ya Wabunge, zikaanza tena kelele… Spika akataja list ya Wabunge wengine ambao wanasimamishwa kuhudhuria Vikao vya Bunge kwasiku tano kila mmoja.

Ezekiel Wenje, Mussa Kombo, Masoud Abdallah Salim, Rebecca Ngodo, Sabrina Sungura,Khatib Said Haji, Dr. Anthony Mbassa, Maulidah Anna Valerian Komu, Kulikoyela Kahigi, Cecilia Pareso, Joyce Mukya, Mariam Msabaha, Grace Kiwelu, Israel Natse, Mustapha Akonaay, Konchesta Rwamlaza, Suleiman Bungura, Rashid Ali Abdallah,Ali Hamad,Riziki Juma,Rukia Kassim Ahmed,Azza Hamad,Khatibu Said Haji,Kombo Khamis Kombo,Ali Khamis Seif,Haroub Mohammed Shamisi,Kuruthum Jumanne,Mchuchuli,Amina Mwidau,Mkiwa Kimwanga,Salum Baruhani,Marry Stellah Malaki,Rashid Ally Omary,Mwanamrisho Abama na Lucy Owenya

Jumatano, 1 Julai 2015

RATIBA YA CECAFA KAGAME CUP

Michuano ya kombe la kagame Cecafa kuanza kutimua vumbi Julai 18 hadi Agosti 2 jijini Dar es Salaam, huku wawakilishi wa Tanzania, Timu ya Yanga ilimepangwa kundi A  na Azam ikiwa imepangwa kwenye kundi C.

Mechi ya ufunguzi tarehe 18 Julai, 2015 Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam itashuhudia wenyeji Yanga SC wakicheza na Gor Mahia ya Kenya, huku APR ya Rwanda ikicheza na Al Shandy ya Sudan na KMKM ya Zanzibar wakifungua dimba na Telecom ya Somalia.

Timu tatu zitakazoshika nafasi ya juu kutoka kundi A, timu mbili za juu kutoka kundi B & C, na mshindi mwenye wastani mzuri kutoka kundi B & C zitaingia katika hatua ya robo fainali.

KUNDI A
YANGA (Tanzania)
GOR MAHIA (Kenya)
KHARTOUM (Sudan)
TELECOM (Djibout)
KMKM (Zanzibar)


KUNDI B
APR (Rwanda)
AL SHANDY (Sudan)
LLB (Burundi)
ELMAN (Somalia)

KUNDI C
AZAM(Tanzania)
MALAKIA(South Sudan)
KCC(Uganda)
ADAMA City (Ethiopia)

LIGI DARAJA LA KWANZA KUANZA KUTIMUA VUMBI SEPTEMBA 12

Ligi Daraja la Kwanza (FDL)  kwa msimu wa 2015/2016 kuanza kutimua vumbi Septemba 12 mwaka huu.
Ligi hiyo itachezwa katika makundi matatu ya timu nane nane kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.

Mfuko huo wa makundi matatu umetokana na marekebisho ya Kanuni za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) yaliyofanywa hivi karibuni na Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) 

Mshindi wa kwanza wa kila kundi atapanda kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kwa msimu wa 2016/2017 wakati timu itakayoshika nafasi ya mwisho katika kila kundi itashuka kucheza Ligi Daraja la Pili (SDL) kwa msimu wa 2016/2017.

Kundi A linaundwa na timu za African Lyon FC (Dar es Salaam), Ashanti United SC (Dar es Salaam), Friends Rangers FC (Dar es Salaam), Kiluvya United FC (Pwani), Kinondoni Municipal Council FC (Dar es Salaam), Mji Mkuu FC (Dodoma), Polisi Dar es Salaam na Polisi Dodoma.

Timu zinazounda kundi B ni Burkina Faso FC (Morogoro), Kimondo SC (Mbeya), Kurugenzi Mafinga FC (Iringa), Lipuli FC (Iringa), Njombe Mji FC (Njombe), Polisi Morogoro na Ruvu Shooting (Pwani).

Kundi C ni Geita Gold SC (Geita), JKT Kanembwa FC (Kigoma), JKT Oljoro (Arusha), Mbao FC (Mwanza), Panone FC (Kilimanjaro), Polisi Mara, Polisi Tabora na Rhino Rangers (Tabora).

WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO


Jumla ya wanafunzi 55,003 wakiwemo wasichana 23,303 na wavulana 31,700 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi kwa mwaka 2015

Wanafunzi waliochaguliwa ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali. Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 29,744 wakiwemo wasichana 11,450 na wavulana 18,294 sawa na asilimia 54.08 watajiunga na masomo ya Sayansi na Hisabati; na wanafunzi 25,259 wakiwemo wasichana 11,853 na wavulana 13,406 sawa na asilimia 45.92 wamechaguliwa kusoma masomo ya Sanaa na Biashara.

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2015 wataanza muhula wa kwanza tarehe 18 Julai, 2015, hiyo ni kwa mujibu wa  Ofisi ya Waziri Mkuu-Tamisemi.



Bonyeza hapa kupata orodha ya wanafunzi waliochaguliwa

Jumanne, 30 Juni 2015

MILLEN MAGESE, EDDY KENZO WAIBEBA EAST AFRICA TUZO ZA BET

tuzo aliotunukiwa Millen
Mwanamitindo na Mrembo wa Tanzania mwaka 2001, Happiness Millen Magese ametunukiwa tuzo ya pekee ya BET mwaka huu iitwayo ‘Global Good Award’
Millen amepewa tuzo hii kutokana na jitihada zake za kampeni ya ugonjwa wa endometriosis (ugonjwa unaosababishwa na seli za tumbo la uzazi kuwa nje ya kizazi) ambao amekuwa nao katika maisha yake yote tangu awe msichana.

Millen ameanzisha taasisi ya kuwasaidia wanawake wengine  hapa nchini ya Millen Magese Faundation ili waepuke kile ambacho kilimkuta yeye. Pamoja na hivyo Millen amekuwa mstari wa mbele kutoa misaada mbalimbali kwa wasiojiweza.

Eddy Kenzo kwenye red carpet akiwa na wapambe
Katika tuzo hizo pia msaani wa Uganda Eddy Kenzo amebeba tuzo ya msanii bora mpya wa kimataifa anayependwa na watazamaji (Viewer’s Choice Best New International Artist, 2015)
Kaitka kipengele hicho Eddy Kenzo alikuwa akichuana na Assper Nyovest wa Afrika kusini, Mz Vee wa Ghana na wasanii wa uingereza, George the poet, MIC Lowry Na Novelist

Kenzo katika ukurasa wake wa facebook amewashukru washabiki wake, huku akisema ilikuwa ni safari ndefu na akasema ni tuzo ya pekee kwa ukanda wa Afrika Mashariki.


Jumapili, 21 Juni 2015

KIBARUA CHA KOCHA NOOIJ CHAOTA NYASI TAIFA STARS

 kocha  wa stars aliyefungashiwa virago, Mart Nooij
Kibarua cha mholanzi Mart Nooij kimefikia tamati baada ya kikao cha  kamati ya utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kulichokaa  kujadili mwenendo wa timu ya taifa, Taifa Stars. Mkataba wa Nooij na Taifa Stars ulikuwa umebakia miezi 10

Pia Kamati hiyo imevunja  benchi la ufundi la timu hiyo mpaka benchi jipya litakapotangazwa.

Kibarua cha Nooij kinafikia tamati baada ya kufuingwa mechi tano mfululizo zikiwemo mechi kati ya Lesotho, Madagascar, Botswana, Misri na mechi ya jana dhidi ya Uganda ambayo Stars imeambulia kipigo cha mabao 3-0 katika uwanja wa Amaan, Zanzibar.

Tangu Nooij aichukue stars April mwaka jana Kutoka kwa Kim Poulsen, ameiongoza timu hiyo katika mechi 18 kati ya hizo ameshinda mechi 3, sare mechi 6, na kufungwa mechi 9



Jumamosi, 20 Juni 2015

KWA MATOKEO HAYA,JE SAFARI YA NOOIJ IMEWADIA?

Erisa Sakimbu mfungaji wa mabao mawili ya The Cranes(picha kutoka Bin Zubery)
MABAO mawili ya mshambuliaji Erisa Sekisambu  wa timu ya taifa ya uganda, the cranes,yanaweza kuwa yamehitimisha historia ya kocha Mholanzi, Mart Nooij katika timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars baada ya kufungwa 3-0 na Uganda usiku huu katika Uwanja wa Amaan, Zanzibar. 

Mchezo huo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza kufuzu michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) itakayofanyika Rwanda mwaka 2016, Sekisambu alimtungua kipa Deo Munishi ‘Dida’ bao moja kila kipindi, wakati bao la tatu lilifungwa na Farouk Miya dakika ya 89.

Mechi hiyo ni ya tano mfululizo Stars kufungwa, baada ya awali kufungwa na Madagascar, Lesotho, Botswana katika michuono ya COSAFA ambayo stars ilishiriki kama mwalikwa, na wiki iliyopita ikaambulia kipigo kutoka kwa misri.

Jumatano, 17 Juni 2015

LIGI KUU UINGEREZA KUTIMUA VUMBI AGOSTI 8

Mabingwa watetezi Chelsea the Blues wataanza kutetea taji lao la ligi kuu katika uwanja wao wa nyumbani wa Stamford Bridge watakapo pambana na Sweswea  katika mechi za ufunguzi zitakazopigwa kati ya Agosti 8-9.

Washindi wa pili Man city wao watasafiri kwenda kuwakabili west bromwich albion, huku majirani zao Machester United wakiwakaribisha Tottenham Old Trafford.

Mabingwa wa kombe la FA Arsenal wao watakuwa nyumbani kuwakaribisha wagonga nyundo wa jiji la London, huku majogoo wa anfield timu ya liverpool watasafiri kwenda kuwakabili

Ijumaa, 12 Juni 2015

LAPTOP ZILIZOTENGENEZWA KENYA

Chuo Kikuu cha Kilimo na technologia cha Jomo Kenyatta Nchini Kenya, JKUAT, leo kimezindua kumputa mpakato iliyotengezwa nchini humo.

JKUAT kwa kushirikaina na wizara ya Viwanda Na Ujasiriamali imezindua laptop hiyo yenye ukubwa wa Corei3, 4GB na 500GB kwa habari zaidi tembelea tuko.co.ke

Dr. Mauki: PATA KUJUA VITU VINGI ILI UWE NA MAMLAKA

                                     Dr.Mauki akiwa na baadhi ya wanafunzi baada ya Mhadhara

Mwalimu na mtaalam wa maswala ya mahusiano Dr.Chris Mauki ametoa rai kwa vijana kujifunza mambo mengi yenye maana na yanayoendana na malengo yao ili waweze kuwa na mamlaka kwa yale wanayoyatenda.

Akizungumza kwenye Mhadhara  katika chuo kikuu cha Tumaini Dar es Salaam. Dr. Mauki amesema kuna njia tano ambazo mtu anaweza kuzitumia kufikia mafanikio na kuwa na mamlaka.

Njia hizo amezitaja kuwa ni pamoja na kutengeneza mtaji wa watu (social capital), kutambua vipawa na talanta ndani ya mtu na kuziendeleza(discover the talent within You), kutimiza majukumu na kuacha uvivu(be responsible and dont be lazy), kuacha kupoteza muda ukitafuta kazi  badala yake kutumia muda kutatua matatizo kwenye jamii(use time effectively to solve problem), na kuepuka wanaokudharau na kuwakumbatia wanaokutia moyo na kukukosoa kwa moyo wa upendo(dont let any discouragement on you, associate yourself with positive critics people).
"huwezi kuwa na mamlaka juu ya jambo kama ujui vitu vingi kuhusu hilo jambo, kipaji pekee akitoshi juhudi inahitajika kuhakikisha unakuwa na mamlaka kwenye kitu ambacho wewe ni bora".

Dr. mauki amesema si jambo la busara kupoteza muda kutaka kutenda bila kuweka juhudi kwenye vitendo, huku akisisitiza wengi wa waliofanikiwa ni watu ambao wamekuwa na macho ya mwewe wakijaribu kuona mbali. kwa kutumia vipawa walivyonavyo.