Katika maisha ni vigumu kukua bila kusikia ili neno,
“maji ni uhai” katika hali halisi ya
dhana maji ni uhai tunaambiwa maji uchukua asilimia kubwa ya mwili wa binadamu
pia maji kwa kiasi kikubwa ndio yamezunguka uso wa dunia.
![]() |
| mkufunzi wa uogeleaji akiwa na wanafunzi katika mazoezi |
Maji ni uhai kwa kuwa mwili wa binadamu una uhuitaji
wa maji pia viumbe hai vyote kwa kiasi kikubwa utegemea maji ili viishi. Lakini
maji pia ni chanzo cha kupotea kwa uhai kwa viumbe hawa ambao utegemea sana
maji.
Dunia imeshuhudia vifo vingi vya maji inapotekea
majanga kama kuzama kwa meli, mashua na boti, lakini pia inapotokea mafuriko. Majanga
haya ugharimu maisha ya watu wengi zaidi. Lakini pia uzembe wa kutofunika
baadhi ya mashimo hama vyombo vya maji navyo vimekuwa vikigharimu uhai.
Kumekuwa na matukio mengi ya watu kudumbukia kwenye
madibwi na kupoteza maisha ila pia watoto majumbani kufariki kwa kudumbukia
kwenye vyombo vyenye maji ama visima.
Kama maji ni uhai je kwa nini vifo hivi vinatokea?
Jibu la swali hili linaweza kuwa gumu kidogo lakini kwa jibu la kawaida ni kuwa
kila chenye uzuri hakikosi ubaya au wengine wanasema ukizidisha kilakitu
kinakuwa sumu.
Maana yake ni kuwa maji yasipotumiwa vizuri yaani
kuchukua tahadhari na kujua hatari za maji bhasi ni chanzo kikubwa cha kupotea
kwa maisha.
![]() |
| boya la kuokolea |
Je vifo vya maji ni mpango wa Mungu?
Stewart Kiluswa mkufunzi wa uogeleaji kwa kujiokoa
na kuokoa maisha, anasema, vifo vingi vya maji hutokea kutokana na uzembe na
kutokujua hatari za maeneo watu wanamoishi au jinsi ya kujioka na hatari za
maji.
Unawezaje kutambua hatari za maji na jinsi gani ya
kujikinga nazo.
Kujua hatari za maji ni vyema kuwa na mwenyeji au
kuuliza wenyeji hali halisi ya mazingira
ya maji uliopo, kama kuna wanyama wakali, mikond mkali wa bahari au kama kuna
alama kataza (zinazozuia) matumizi ya eneo hilo. Pia kuwa waangalifu na vyombo
vya maji kama ndoo na baseni hasa hasa tunapokuwa na watoto wadogo, pia
kuhakikisha mazingira yetu yenye mashimo makubwa yanawekea alama za tahadhari
ili kuzuia majanga. Mara nyingi watoto upenda kwenda kucheza wakiwa peke yao ni
vyema kujua wanachezea maeneo gani na kama ni eneo la maji ni vyema wakawa na
uangalizi wa mkubwa.
![]() |
| mmoja wa wanaojifinza kuogelea |
Jinsi ya
kujiokoa na kuokoa mtu aliye katika hatari ya kufa maji.
Kuna aina ya watu wane wanaokuwa katika hatari ya
kufa maji nao ni:
Asiyejua kuogelea kabisa, anayejua kuogelea kidogo,
anayejua kuogelea na aliyepoteza fahamu
majini
Asiyejua kuogelea huyu mara nyingi akiwa katika hatari ya kufa
maji huzama na kuibuka akiwa katika hali ya wima, ilihali anayejua kuogelea
kidogo huzama na kuibuka akiwa katika hali ya mshazali na mara nyingi
hujitahidi kuelekea sehemu ambayo anaweza kupata musaada kwa haraka, huyu
ujitahidi kujaribu kuogelea ndio maana huwa
katika hali ya mshazali.
Anayejua kuogelea, anaweza kuwa katika hatari ya
kufa maji kutokana na sababu kama kushambuliwa na wanyama au wadudu wa majini
na hvyo akili yake yote uhiamishia palipo na jeraha ila pia anaweza kuwa
amebanwa na matatizo ya msuli hivyo vyote vinaweza kupelekea maisha ya mtu kuwa
hatarini kwenye maji.
Aliyepoteza fahamu huyu ni kwamba anakuwa ajitambui
na mwili wake unaweza kuwa unaelea au umezama chini.
Wakati wa kuwapatia msaada wa uokozi jitahidi sana
kutokumgusa mtu ambaye bado ni mzima yaani ajapoteza fahamu. Tumia nyenzo
yoyote ile ambayo ataweza kuishika na ww kumvuta kwa kutumia hyo nyenzo, mfano
wa nyezo za uokozi ni kama maboya, mti
mrefu, kamba au kidumu chenye mfuniko kilichofugwa kamba au nguo au kitu
chochote kinachoelea, kumbuka wakati unajaribu kuokoa hakikisha maisha yako ni
salama. Kwa mtu ambaye amepoteza fahamu unaweza kumfikia na kumshika wakati wa
kumtoa kuelekea nchi kavu.
Maji ni uhai ila pia maji ni chanzo cha vifo,
tujihadhari katika matumizi ya maji.



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni