Jumamosi, 11 Julai 2015

MMOJA ASHIKILIWA NA POLISI KUELEKEA MKUTANO MKUU CCM

Polisi Dodoma inamshikilia mtu mmoja mwenye asilia ya Asia akiwa na kiasi kikubwa cha fedha, ahusishwa na mchakato wa mchujo unaondelea.
Raia anaedaiwa kukamatwa, pamoja na fedha alizokutwa nazo

katika mitandao ya kijamii picha za mtu huyo zimesambaa sana huku akihusishwa na mmoja wa wagombea walio katika tano bora, Bernard Membe.

Akielezea sintofahamu hiyo, Bernard Membe ameandika katika ukurasa wake wa twitter akisema, "Kuna taarifa za uongo zinazoenezwa kwamba kuna "Mtu wa Membe" amekamatwa na pesa Dodoma,siasa hizi ni za hovyo kwani hazitajenga Taifa letu. Naomba msihadaike na watu wanaotaka kututia doa baada ya kukosa uchafu dhidi yetu"

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni