Jumanne, 7 Julai 2015

MBUNGE CHADEMA ANUSURIKA, AJALI YA HELIKOPITA

helikopita baada ya kuanguka.
Mbunge wa Arumeru Mashariki,mkoani Arusha Joshua Nassari amepata ajali ya helkopta aliyokua anaitumia kufanya ziara katika jimbo lake.

Habari za awali tulizozipata ni kwamba mbunge huyo wa Chadema Joshua Nassari amenusurika kufa baada ya Helkopta aliyokuwa anaitumia kuanguka baada ya kunasa kwenye mti baada ya kupotea kwenye mawingu.


Aidha taarifa hizo zinaeleza kuwa Mbunge huyo kwa Tiketi ya Chadema, na rubani wake walitoka wakiwa wazima na wapo katika Hospitali ya Kanisa la Kilutheri ya Selian ya jijini Arusha. 
Mbunge wa Arumeru mashariki, Joshua Nassari akiwa na helicopita aliyopata nayo ajali

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni