Ijumaa, 12 Juni 2015

Dr. Mauki: PATA KUJUA VITU VINGI ILI UWE NA MAMLAKA

                                     Dr.Mauki akiwa na baadhi ya wanafunzi baada ya Mhadhara

Mwalimu na mtaalam wa maswala ya mahusiano Dr.Chris Mauki ametoa rai kwa vijana kujifunza mambo mengi yenye maana na yanayoendana na malengo yao ili waweze kuwa na mamlaka kwa yale wanayoyatenda.

Akizungumza kwenye Mhadhara  katika chuo kikuu cha Tumaini Dar es Salaam. Dr. Mauki amesema kuna njia tano ambazo mtu anaweza kuzitumia kufikia mafanikio na kuwa na mamlaka.

Njia hizo amezitaja kuwa ni pamoja na kutengeneza mtaji wa watu (social capital), kutambua vipawa na talanta ndani ya mtu na kuziendeleza(discover the talent within You), kutimiza majukumu na kuacha uvivu(be responsible and dont be lazy), kuacha kupoteza muda ukitafuta kazi  badala yake kutumia muda kutatua matatizo kwenye jamii(use time effectively to solve problem), na kuepuka wanaokudharau na kuwakumbatia wanaokutia moyo na kukukosoa kwa moyo wa upendo(dont let any discouragement on you, associate yourself with positive critics people).
"huwezi kuwa na mamlaka juu ya jambo kama ujui vitu vingi kuhusu hilo jambo, kipaji pekee akitoshi juhudi inahitajika kuhakikisha unakuwa na mamlaka kwenye kitu ambacho wewe ni bora".

Dr. mauki amesema si jambo la busara kupoteza muda kutaka kutenda bila kuweka juhudi kwenye vitendo, huku akisisitiza wengi wa waliofanikiwa ni watu ambao wamekuwa na macho ya mwewe wakijaribu kuona mbali. kwa kutumia vipawa walivyonavyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni