| kocha wa stars aliyefungashiwa virago, Mart Nooij |
Kibarua cha mholanzi Mart Nooij kimefikia tamati baada ya
kikao cha kamati ya utendaji ya Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kulichokaa kujadili mwenendo wa timu ya taifa, Taifa Stars.
Mkataba wa Nooij na Taifa Stars ulikuwa umebakia miezi 10
Pia Kamati hiyo imevunja
benchi la ufundi la timu hiyo mpaka benchi jipya litakapotangazwa.
Kibarua cha Nooij kinafikia tamati baada ya kufuingwa mechi
tano mfululizo zikiwemo mechi kati ya Lesotho, Madagascar, Botswana, Misri na
mechi ya jana dhidi ya Uganda ambayo Stars imeambulia kipigo cha mabao 3-0
katika uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Tangu Nooij aichukue stars April mwaka jana Kutoka kwa Kim
Poulsen, ameiongoza timu hiyo katika mechi 18 kati ya hizo ameshinda mechi 3,
sare mechi 6, na kufungwa mechi 9
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni