Jumatano, 1 Julai 2015

WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO


Jumla ya wanafunzi 55,003 wakiwemo wasichana 23,303 na wavulana 31,700 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi kwa mwaka 2015

Wanafunzi waliochaguliwa ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali. Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 29,744 wakiwemo wasichana 11,450 na wavulana 18,294 sawa na asilimia 54.08 watajiunga na masomo ya Sayansi na Hisabati; na wanafunzi 25,259 wakiwemo wasichana 11,853 na wavulana 13,406 sawa na asilimia 45.92 wamechaguliwa kusoma masomo ya Sanaa na Biashara.

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2015 wataanza muhula wa kwanza tarehe 18 Julai, 2015, hiyo ni kwa mujibu wa  Ofisi ya Waziri Mkuu-Tamisemi.



Bonyeza hapa kupata orodha ya wanafunzi waliochaguliwa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni